Na Mwandishi wetu,Shinyanga
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Patrobas Katambi amesema hajavunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Kupiga Marufuku Mikutano ya siasa nchini huku akisema hayuko tayari kuona Taifa linaangamia kwa kuacha kundi la watu wachache wenye maslahi binafsi ambalo linakiuka haki za wananchi wengi.
Ameyasema hayo wakati akizungumza na mamia ya wazee na wanachama wa Baraza la Ushauri la Wazee la Manispaa ya Shinyanga, katika maadhimisho ya Siku ya kupinga Ukatili dhidi ya Wazee Duniani yaliyofanyika leo mkoani Shinyanga

0 Comments